Mwanamuziki mkongwe nchini, Cosmas Chidumule, amesema muziki wa dansi hauna nidhamu na ndiyo maana ameamua kuachana nao baada ya kuokoka ili amrudie Mungu.
Chidumule aliyasema hayo hivi karibuni, jijini Dar es Salaam, kuwa mara nyingi wanamuziki wa dansi na wengineo thamani yao inakuwa ndogo mbele ya hadhira.
Alisema wengineo hufika mbali kwa kuamua kuwatuza waimbaji bangi au vitu vingine visivyokuwa na manufaa katika maisha yao, jambo ambalo ameamua kuachana nalo.
“Huu ni wakati wa kumrudia Mungu, maana si mara zote waimbaji wanakuwa na thamani kwa mashabiki wao na ndiyo maana baadhi yao wanatunzwa bangi,” alisema.

0 comments:
Post a Comment