Tuesday, September 24, 2013

Saa 51 za mapambano


By on 12:49 AM

Westgate, zimeshuhudia jana milio mizito ya risasi na mabomu kutoka ndani ya jengo hilo. Mapambano kati ya askari wa vikosi vya ulinzi na usalama vya Kenya, yalipamba moto jana mchana na kusababisha moshi mzito kutoka ndani ya jengo hilo.

Tukio hilo lilitokea baada ya askari wa kikosi maalumu cha Kenya, wakisaidiwa na maofisa usalama kutoka nchi za Israel, Marekani na Uingereza, kuanza kazi ya kuwafikia wanamgambo wa Kiislamu wa Al-Shabaab. Waziri wa Mambo ya Ndani, Joseph Ole Lenku, alisema katika mapambano hayo, magaidi wawili waliuawa na mateka kadhaa waliokolewa.

“Wanamgambo wote ni wanaume, japokuwa baadhi walivalia kama wanawake.

“Tunadhani operesheni itafikia mwisho muda si mrefu,” alisema. “Tunadhibiti sakafu zote, magaidi wanakimbia na kujificha katika baadhi ya maduka. Hakuna sehemu ya kutorokea,” alisema Waziri Lenku.

Alisema kuna hofu idadi ya vifo huenda ikaongezeka, wakati askari wakiendelea kutafuta watu walionusurika na miili katika maeneo mbalimbali ya maduka.

Alisema karibu mateka wote wameokolewa kutoka jengo hilo, saa chache bada ya kukumbwa na mlolongo wa mashambulizi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi, David Kimaiyo, alisema katika ujumbe wake wa Twitter kuwa katika siku ya tatu ya shambulio hilo, waliwaokoa mateka baada ya kuingia jengoni huku wakizidi kupata mafanikio dhidi ya washambuliaji.

Alisema jana mchana, kuna watu kadhaa waliokamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Nairobi, wakijaribu kutoroka.


About Syed Faizan Ali

Faizan is a 17 year old young guy who is blessed with the art of Blogging,He love to Blog day in and day out,He is a Website Designer and a Certified Graphics Designer.

0 comments:

Post a Comment