Msanii wa filamu nchini, Nice Mohamed ‘Mtunisi’, amesema baadhi ya wasanii wa filamu nchini, wana tabia ya kubagua wenzao katika kila shughuli zinazohitaji umoja wao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Mtunisi alisema tabia hiyo itajenga chuki na kupunguza idadi ya wasanii kuhudhuria vikao na shughuli zinazohitaji umoja wao ili zifanikiwe.
“Siku hizi hakuna upendo wala ushirikiano kati yetu wasanii, wengi wana ubinafsi na hawajali wenzao, kwa mtindo huu hatuwezi kufikia mafanikio. Inatupasa tushirikiane kwa upendo wa kweli na si unafiki,’’ alisema Mtunisi.

0 comments:
Post a Comment